NENO LA SHUKRANI KUTOKA KWA MWENYEKKITI WA KLABU YA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA LINDI (LRPC).

 


NENO LA SHUKRANI KUTOKA KWA MWENYEKITI.

Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa  Lindi, Fatuma Maumba,  anapenda kutumia fursa hii kutoa shukrani za dhati kwa upendo, faraja, na msaada mkubwa ambao tumeupokea kutoka kwenu na wengine wote ambao mmetusaidia katika wakati huu mgumu wa kuwapoteza wapendwa wetu, Abdallah Nanda (Channel ten) na Josephine Kibiriti (Star Tv) ambao walikuwa wawakilishi mkoa wa Lindi.

Naomba nitoe shukrani za pekee kwa wale ambao walitoa mchango wao wa kifedha na kumkabidhi Mwenyekiti kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa Lindi, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, CCM mkoa wa Lindi, Mama Salma Kikwete, Bodi ya korosho, Chama cha ushirika Lindi Mwambao, Bandari ya Mtwara (PTA), Ofisi ya Mganga Mkuu mkoa wa Lindi na wadau wote waliotoa mmoja mmoja. Upendo wenu umetupa nguvu na kutufanya tujisikie wenye bahati kuwa na marafiki kama nyinyi.

Tunamuomba Mwenyezi Mungu awape nguvu na faraja katika maisha yenu na awape amani tele. Tuna imani kwamba wapendwa wetu sasa wapo mahali pema na amani ya milele.

Tena, shukrani nyingi kwa wote ambao wamekuwa pamoja nasi wakati huu wa majonzi. Mwenyezi Mungu awabariki nyote.

Kwa upendo na shukrani tele,

Fatuma Maumba

Mwenyekiti

Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Lindi (LRPC).

Post a Comment

0 Comments